tag:blogger.com,1999:blog-78167877361334705942024-03-05T05:51:53.927-08:00Mwanamalenga.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.comBlogger14125tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-54009723061186926342012-02-14T17:40:00.000-08:002012-02-14T17:56:00.989-08:00NyotaWaridi nakutafuta, shairi niliandika,<br />Siku nazo zikapita, mwandani nilimsaka, <br />Sasa nimeshampata, wakati umeshafika,<br />Nyota wangu unang'aa, daima nitakupenda.<br /><br />Nyota unanisikia, ninakupenda kwa dhati,<br />Thamaniyo naijua, ya dhahabu haikuti,<br />Kuwa nawe najivunia, daima wala sijuti,<br />Nyota wangu unang'aa, daima nitakupenda.<br /><br />Ukitaka nitafune, ukitaka unimeze,<br />Utamuwo wa senene, Wahaya na waeleze,<br />Si mwembamba si mnene, wa wastani nikujuze,<br />Nyota wangu unang'aa, daima nitakupenda.<br /><br />Asante kwa kunijali, thamani kubwa wanipa,<br />Hujanipenda kwa mali, mapungufu hujakwepa,<br />Tupitazo zote hali, hutanitenga 'meapa,<br />Nyota wangu unang'aa, daima nitakupenda.<br /><br />Washibisha nafsi yangu, Nyota nakuambia,<br />Waujaza moyo wangu, kwa penzi 'lilotimia,<br />Heko malaika wangu, kwa penzi li'lotulia,<br />Nyota wangu unang'aa, daima nitakupenda.<br /><br />Nyota ninamaanisha, Stella maana yake,<br /> Urembo usiokwisha, hii sifa yake,<br />Nakupenda wa maisha, ujumbe hima ufike,<br />Nyota wangu unang'aa, daima nitakupenda.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com2tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-33942715942091618062011-12-23T06:38:00.001-08:002011-12-23T06:56:24.405-08:00Laiti angekuwepoKauli i'lozagaa, ya tamaa kuikata,<br />U wapi u'lotufaa, twatamani kukufwata,<br />Nchi inachechemea, ni mengi yanatukuta,<br />Laiti angekuwepo, mbona Kingunge tunaye?<br /><br />Ngombale bado tunaye, hima tumtumieni,<br />Nyerere hatupo naye, fikra'ze zipo vichwani,<br />Busara'ze ajuaye, Kingunge hoja mezani.<br />Laiti angekuwepo, Mama Nyerere tunaye.<br /><br />Mama yetu wa Taifa, ana mengi kutufunza,<br />Laiti hii ni kashfa, mama bado anaweza,<br />Kujuta wala si sifa, busara'ze si kubeza,<br />Laiti angekuwepo, Malecela mbona yupo? <br /><br />Tokea enzi za baba, alikuwapo Msuya,<br />Busara alizishiba, wala takrima hakula,<br />Mbinu bado kazibeba, atumiwe bila hila,<br />Laiti angekuwepo, mbona wengi bado wapo?<br /><br />Hebu tuwape nafasi, historia wapakue, <br />Makovu yake nanasi, utamu'we palepale,<br />Tuache mawazo hasi, wazee wasaidie,<br />Laiti angekuwepo, wapo tuwatumieni.<br /><br />Laiti si neno zuri, twende mbele Tanzania,<br />Uzalendo ndio siri, tujibidishe kwa nia,<br />Bila Nyerere si shwari, msemo wa mazoea,<br />Laiti angekuwepo, mawazoye twatumia?<br /><br />Wapo wengi wa zamani, enzi zile za Mwalimu,<br />Ni wachache shairini, wote kuwepo ni ngumu,<br />Tupeni dira jamani, wa mwalimu mu muhimu,<br />Laiti angekuwepo, Mpo wengi m'lo tunu.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com2tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-85802123430882927652011-05-20T04:25:00.000-07:002011-05-22T00:48:52.573-07:00Ajali zaepukika!Jamani nisikizeni, nisomeni waungwana,<br />Nafichani moyoni, lipi lisojulikana,<br />Ajali tele pomoni, usiku hata mchana,<br />Madereva mwahusika, ajali zaepukika.<br /><br />Wa mabasi wamiliki, amueni mtaweza,<br />Andaeni mikakati, ajali kutokomeza,<br />Magari muyahakiki, kabla safari kuanza.<br />Madereva yao haki, wapeni bila kupinda.<br /> <br />Ulevi na muuache, madereva mwahusika.<br />Subiri hima kukuche, usiku hamtafika.<br />Sheria mzitumie, mnazitambua fika.<br />Madereva mtulie, ajali zaepukika.<br /><br />Ajali zimekithiri, za mabasi si kificho,<br />Vita si ya hiari, fungueni yenu macho,<br />Maisha ya wasafiri, bora ya mboni ya jicho,<br />Kukumbushwa msisubiri, ajali zaepukika.<br /><br />Abiria kataeni, mwendo uliomkali,<br />Roho zenu teteeni, si budi kuwa wakali,<br />Mikanda katika siti, fungeni kwa kila hali.<br />Wasafiri unganeni, uhai wenu chungeni.<br /><br />Polisi barabarani, mwahusika siwafichi,<br />Rushwa sasa acheni, wateteeni wananchi,<br />Magari ya'lo walakini, hakikisha huyaachi.<br />Usalama dumisheni, ajali 'taepukika.<br /><br />Wasanii Five Star, walipoteza maisha,<br />Ajali twakumbukia, uzembe lisababisha,<br />Mv bukoba nakumbushia, uzembe umetutosha,<br />Meli ilielemea, ukweli sitopindisha.<br /><br />Amani umetutoka, Kessy tulikuhitaji,<br />Tunalia tunachoka, ajali "mekuwa jaji,<br />Ajalini 'mekufika, mauti yasotaraji,<br /> Ajali 'metunyang'anya, rafiki yetu mkubwa.<br /><br />Abiria ushikeni, huu wangu ushauri,<br />Kulala na epukeni, pindi mnapo safiri,<br />Magazetini kunani, iwe mwisho wa safari.<br />Hakuna jipya fanani, yote nayakariri.<br /><br />Sina tena la ziada, zinaepukika ajali,<br />Hebu hii iwe mada, namna ya kukabili,<br />Uhai vema kulinda, tena kwa hali na mali.<br />Janga si la kawaida, tujipange kukabili.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com7tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-2985942987439245712010-10-04T07:21:00.005-07:002010-10-04T07:21:23.710-07:00Joka mbona huzeeki?Upo toka Tanganyika, hadi sasa Tanzania,<br />Msingi aliuweka, baba kesha tangulia,<br />Tayari tungeshafika, Nyerere angendelea,<br />Joka mbona huzeeki, binafsi nimekuchoka.<br /> <br />Chumvi yote ulokula, tumia basi busara,<br />Ifike tena pahala, hima iamue kura,<br />Watu ndio wenye hila, chombo hakina papara,<br />Joka mbona huzeeki, binafsi nimekuchoka.<br /><br />Wajengao hicho chombo, kizalendo watafteni,<br /> Ndani kimejaa shombo, chaoshwa kwenye kampeni,<br />Waambulia kikumbo, watetezi wa maskini,<br />Joka mbona huzeeki, binafsi nimekuchoka.<br /><br />Kalamu ninaiacha,wino kamwe hutokwisha,<br />Joka ondoa makucha, malengo kufanikisha,<br />Tazama panavyokucha, huna budi kutupisha,<br />Joka mbona huzeeki, binafsi nimekuchoka.<br /><br />Uzee busara bwana, zeeka inakubidi,<br />Kwanini unang'ang'ana , twajua ushafaidi, <br />Wapeni nao vijana, tuifikie ahadi,<br />Joka mbona huzeeki, binafsi nimekuchoka.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com1tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-2302246308084589232010-03-29T10:34:00.001-07:002010-03-29T10:41:31.245-07:00Nakutafuta amani.Ajali kila uchao,maisha yanapotea,<br />wapo wengi hatunao,kwa mola wametangulia,<br />viongozi soni kwao,lawama twawatupia,<br />Nakutafuta amani,waongewa sikuoni.<br /><br />Rushwa iliyokithiri,masikini waonewa,<br />wakubwa wanakiburi,uchumi wahujumiwa,<br />pesa kitu jeuri,sheria yapinduliwa,<br />Nakutafuta amani,waongewa sikuoni.<br /><br />Ufisadi wabobea,wahusika wanafichwa,<br />serikali inawajua,majina wanatunziwa,<br />chamani waogelea,uswahiba twaelewa,<br />Nakutafuta amani,waongewa sikuoni.<br /><br />Maji ni kubwa tatizo,watu wanahangaika,<br />umbali sio mchezo,kina mama wanachoka,<br />umeme bado gumzo,ni lini taimarika,<br />Nakutafuta amani,waongewa sikuoni.<br /><br />Elimu iliyo duni,watoto wataabika,<br />wanakaa mavumbini,kwa shida wanaandika,<br /> viongozi amkeni,kuonewa tumechoka,<br />Nakutafuta amani,waongewa sikuoni.<br /><br />Maisha yaliyo bora,maneno yatamkika,<br />walitaka hizo kura,kapuni wakatuweka,<br />twaishi kama chokora,na siku zinakatika,<br />Nakutafuta amani,waongewa sikuoni.<br /><br />Hii Tanzania yangu,yenye wingi wa maneno,<br />amani hili ni jungu,lakwaza si mfano,<br />amani wapi wandugu,latumika ka'ndoano,<br />Nakutafuta amani,waongewa sikuoni.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com2tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-19838341130275775692009-12-20T05:44:00.000-08:002009-12-20T05:51:49.374-08:00Waridi.Ua ninakutafuta, tayari ushachanua,<br />Marashi nanayapata,manukato yavutia,<br /> Ni lini nitakupata,uzuri najivunia,<br />Waridi nakutafuta, nataka kujichumia.<br /><br /><br />Niite unionapo, wala usibabaike,<br />Sijui wapi ulipo,paza sauti iskike,<br />Ipi ni njia mkato, haraka mimi nifike,<br />Waridi nakutafuta, nataka kujichumia.<br /><br /><br />Ni mengi ninayaona, maua ya kupendeza,<br />Ni lipi lililonona,si kazi ya kubeza,<br />Waridi ndo lanikuna,ua litaniliwaza,<br />Waridi nakutafuta, nataka kujichumia.<br /><br /> Waridi ninakusaka,wa maisha jitokeze,<br />Mbali pia nitafika,ulipo wewe nijuze,<br />ua umeshapevuka,nakuchuma nikutunze,<br />Waridi nakutafuta, nataka kujichumia.<br /><br />Bustanini ninapita,tayari kujichumia,<br />Tabia itanivuta,ua kufuatilia,<br />Najua nitalipata,maisha tafurahia.<br />Waridi nakutafuta, nataka kujichumia.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com2tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-24631185928637594152009-10-09T06:40:00.001-07:002009-10-09T06:40:43.418-07:00MaishaMaisha kweli ni fumbo,lilogumu kufumbua,<br />Leo lakupiga kumbo,kesho wachekelea,<br />Punde yezaenda kombo,sharti kujikwamua,<br />Maisha ndivyo yalivyo,ya kesho huwezi jua.<br /><br /><br />Maisha yamesheheni,uzuri pia ubaya,<br />Ungalipo duniani,usiyaonee haya,<br />Popote yatafuteni,msichoke kusakanya,<br />Maisha ndivyo yalivyo,ya kesho huwezi jua.<br /><br /><br />Usitukane wakunga,na uzazi bado upo,<br />Mlango utafunga,ungali ndani haupo,<br />Meli maisha tasonga,taachwa hapo ulipo.<br />Maisha ndivyo yalivyo,ya kesho huwezi jua.<br /><br /><br />Njiani utayakuta,majabali vizingiti,<br />Huna budi kuyapita,viunzi havikwepeki,<br />Kamwe hakuna kujuta,maisha nasbu bahati,<br />Maisha ndivyo yalivyo,ya kesho huwezi jua.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com2tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-40552289364417349022009-09-21T11:18:00.001-07:002009-09-21T11:18:30.347-07:00MajutoMtegoni nimekwama,pa kutokea sioni,<br />Pande zote natazama,mkombozi simuoni,<br />Ndugu zangu wanisema,msaada siuoni,<br />Siku zangu nazipima,walimwengu kwaherini.<br /><br /><br />Nahara na kutapika,mwili wote ni vidonda,<br />Nywele nazo zanyonyoka,natisha nilivyokonda,<br />Mwili wote unanuka,mauti siwezi shinda,<br />Saa yangu imefika,najuta niliyotenda.<br /><br /><br />Ni wengi watafuata,nakiri nilisambaza,<br />Wengine wameshapita,wengine wazidi cheza,<br />Wasomi niliwachota,fukara sikubakiza,<br />Kweli leo ninajuta,nsamehe Mola muweza.<br /><br /><br />Jamaa wamenitenga,ndugu waninyanyapaa,<br />Mawazo yananisonga,kutengwa kunaniua,<br />Lini kusema ntafunga,wote siku wangojea,<br />Maji yashazidi unga,mauti yanyemelea.<br /><br /><br />Kwa macho hutamuona,unene sio kigezo,<br />Vijana mliopona,hima acheni mchezo,<br />Gonjwa lipo kila kona,acheni vitu vya dezo,<br />Nakufa bado kijana,kwa Mungu mimi chukizo.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com4tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-16601073894463730772009-09-11T03:32:00.001-07:002009-09-11T03:37:43.137-07:00Jua ni la utosini.Asubuhi kunakucha,na njia ninaishika,<br />Ninapokwenda naficha,'tasema ntakapofika,<br />Nitapata ya mchicha?,swali liso na hakika,<br />Jua ni la utosini,linachoma si utani.<br /><br /><br />Ni wangu tena ujio,fungua pesa upate,<br />Chanuo na mafagio,ina njoo nikupake,<br />Anjifu na mitandio,mikufu pia na pete,<br />Jua ni la utosini,linachoma si utani.<br /><br /><br />Huruma siku yapita, ndururu sijainusa,<br />Watoto mimi najuta,viumbe waso na kosa,<br />Mitaa ninaipita,wateja spati kabisa,<br />Jua linanifuata,katu halitaki susa,<br />Jua ni la utosini,linachoma si utani.<br /><br /><br />Machinga ndo kazi yangu,mtaa hadi mtaa,<br />Kazi yanipa machungu,ila sikati tamaa,<br />Nachoka haki ya Mungu,umande nilikimbia.<br />Jua ni la utosini,linachoma si utani.<br /><br /><br />Mlo bahati someni, mwenzenu nilichezea,<br />Chenga nyingi shuleni,vitabu sikushangaa,<br />wasomi mataikuni,tuso skuli twaduwaa.<br />Jua ni la utosini,linachoma si utani.<br /><br /><br />Siombee umachinga,miguu yote yauma,<br />Bora jela kutinga,jua la utosi noma,<br />Pesa haujaichanga,fasta jua lishazama.<br />Jua ni la utosini,linachoma si utani.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com4tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-36669128268638309802009-09-05T22:00:00.001-07:002009-09-05T22:00:17.965-07:00Wosia wa BabuWajukuu sikizeni,muda wangu umekwisha.<br />Leo nimewaiteni, muhimu kuwasilisha.<br />Sikiliza kwa makini,wala sitaki wachosha.<br /><br /><br />Mkamateni elimu,msimwache aendeze.<br />Hii ni nguzo muhimu,ili maisha uweze.<br />Hili ni langu jukumu,nawasihi muutunze.<br /><br />Cha mwenzako si cha kwako,hilo sharti mlijue.<br />Tumia akili yako,muulize kapataje.<br />Kuiba na iwe mwiko,kwa jasho jitafutie.<br /><br /><br />Kweli kuweni makini,gonjwa lipo mtaani.<br />vya dezo kataeni,misaada tambueni.<br />'Siishi kwa tumaini,hasara tele nyumbani.<br /><br />Maisha si lelemama,juhudi inawapasa.<br />Msikubali kukwama,sekunde hata lisaa.<br />Pande zote na tazama,pa kuanza hutokosa.<br /><br />Kueni wavumilivu,matatizo yakabili.<br />Katu msiwe wavivu,msibaki na kandili.<br />Msile ulo mkavu,tulia penye kivuli.<br /><br /> Nguvu zinaniishia,nilosema yashikeni,<br />Huu ndo wangu wosia,ushikeni akilini.<br />Dunia itawambia,pembueni kwa makini.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com3tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-45266043502369533582009-07-31T07:37:00.001-07:002009-07-31T07:37:43.860-07:00Dini zetu ni kikwazo.Mola nakupa heshima,ulimwengu uliumba.<br />leo mimi natazama,wapo waloshayafumba.<br />Kisa wazi nakisema,mimi na wangu mchumba.<br />dini zetu ni kikwazo,e Mola tusaidie.<br /><br /><br />Sio siri nampenda,shairi nimeandika.<br />kwa mwingine sitoenda,mistari niliishuka.<br />vishawishi nitashinda,nilisema na hakika.<br />dini zetu ni kikwazo, e mola tusaidie.<br /><br /><br />Mapenzi hayana dini,kabila wala hayana.<br />semi hizi kulikoni,hatarini kuachana.<br />ya kweli yangu imani,kamwe siwezi ikana.<br />Mwenzangu yake imani,msimamo kesha weka.<br />dini zetu ni kikwazo, e Mola tusaidie.<br /><br /><br />Wazaziwe wamfunza,kiburi wamjazia.<br />dini yake kuitunza,msimamo wamwekea.<br />wazaziwe wanibeza,kifupi wanichukia.<br />dini zetu ni kikwazo, e Mola tusaidie.<br /><br /><br />Baba mama walionya,kupenda kuliniteka.<br />Tayari walishaona,uzoefu 'litumika.<br />yakwao sikuyaona,kupenda kulifunika.<br />Dini zetu ni kikwazo, e Mola tusaidie.<br /><br /><br />Mwanangu hebu tulia,wa diniyo tampata.<br />chunga kutokujutia,matatizo tayapata.<br />haya nayakumbukia,rafiki alinisuta.<br />dini zetu ni kikwazo, e Mola tusaidie.<br /><br /> <br />Njia panda bado nipo,sina pa kuelekea.<br />Nipeni njia mkato,mapenzi nayajutia.<br />Hima popote ulipo,ushauriwo "tapokea.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com3tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-91206737114725192462009-07-24T03:53:00.000-07:002009-07-24T04:00:04.028-07:00Sio siri nakupenda.Miaka ilishapita,magumu niliyavuka.<br />Visiki nilivipita,wa maisha kumsaka.<br />Nilijua 'tampata,papara sikuzitaka.<br />Sio siri nakupenda,kwa mwingine sitoenda.<br /><br /><br />Natamani uwe wangu,niambie nitulie.<br />Ilikuwa siri yangu,imebidi nikujuze.<br />Niwambie ndugu zangu,baraka watujalie.<br />Sio siri nakupenda, kwa mwingine sitoenda.<br /><br /><br />Usiku hata mchana,nakuwaza nisikie.<br />Mapenzi yalomapana,nipokee unifiche.<br />Sio leo wala jana,penzi langu litambue.<br />Sio siri nakupenda,kwa mwingine sitoenda.<br /><br /><br />Sina sababu kupenda, ulivyo waniridhisha.<br />Sitake mimi kukonda,wewe ndo yangu maisha.<br />Naapa sitokutenda,hima sitobabaisha.<br />sio siri nakupenda, kwa mwingine sitoenda.<br /><br /><br />Tamati nimeifika,nambie unachowaza.<br />Kwako nimefika,sijui kama wakwanza.<br />Wewe utachotamka,moyoni tanituliza.<br />Sio siri nakupenda, kwa mwingine sitoenda.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com2tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-4759752552138512422009-07-16T22:19:00.000-07:002009-07-16T22:28:46.746-07:00YATIMA JAMA HURUMA.Yatima waso hatia,huruma napowakuta.<br />mlo wajitafutia,si hakika kuupata.<br />jalalani kuchokona,chochote watachopata.<br />yatima jama huruma,sio lao kusudio.<br /><br /><br />Magonjwa yawaandama,hakuna wa kuwatibu.<br />nani wa kuwatazama,maradhi yawaadhibu.<br />na chawa wawaandama,malazi yaso adabu.<br />yatima jama huruma,sio lao kusudio.<br /><br /><br />Mikononi mwa polisi,mkong'oto kama kazi.<br />maisha ya wasiwasi,watumiwa kwenye wizi.<br />zawakosa na risasi, kifo kipo waziwazi.<br />yatima jama huruma,sio lao kusudio. <br /><br /><br />Wengine pia hubakwa,ukimwi rahisi kupata.<br />Wengine hulawitiwa,makubwa na huwakuta.<br />miili yao yauzwa,<br />wengine kunufaika.<br />Yatima jama huruma, sio lao kusudio.<br /><br /><br />Wazazi nisikieni,tulieni msiruke,<br />ukimwi upo jamani,chunga usiwamalize.<br />malezi ni ya wazazi, walimwengu wako bize.<br />yatima jama huruma, sio lao kusudio.<br /><br /><br />Vijana siwasahau,kila jambo na wakati.<br />katu usijisahau,kuzaa kabla wakati.<br />wala usijejaribu,ngono siipe nafasi.<br />yatima jama huruma,sio lao kusudio.<br /><br /><br />Yapo mengi yawasibu,siwezi yote eleza.<br />Sote na tunawajibu,kutoa tunachoweza.<br />Elimu kwao muhimu,hamasika kuwatunza.<br />Yatima jama huruma, sio lao kusudio.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com3tag:blogger.com,1999:blog-7816787736133470594.post-38267607780238480822009-07-14T00:49:00.000-07:002009-07-14T00:50:32.461-07:00NINI WAMETUFANYIA?Uchaguzi mbili kumi,huo hapo wajongea.<br /> Waja kuisaka kumi, wako waliolowea.<br />wametufanyia nini, jibu sharti kutupatia.<br />tuamke wajameni,tuchague wa kutusaidia.<br />Kura fika haki yako,umpendaye mchague.<br />hupotezi muda wako,uhakika wa badae.<br />nini wametufanyia,waulizwe bila woga.<br /><br />Tarehe itawadia,kampeni kuzipiga.<br />Waongo utawajua,'tazijua zao soga.<br />uwezo kuzingatia, zawadi wakizimwaga.<br />nini wametufanyia,waulizwe bila woga.<br /><br /><br />Takrima usikubali,mzalendo 'ndo kigezo.<br />yule atayekujali, hela isiwe kigezo.<br />Usiukubali wali,wala tisheti za dezo.<br />nini wametufanyia,waulize bila woga.<br /><br /><br />Wageni watatujia,yakwao watatwambia.<br />nini watatufanyia,bayana kutuwekea.<br />zipi 'takuwa hatua,wasipotutimizia?<br />nini wametufanyia,waulizwe bila woga.<br /><br />Kalamu naweka chini,jamani tuwe makini.<br />somo lipo akilini,mitano hiyo ni mingi.<br />nne moja fomesheni,kamchezo kasomeni.<br />nini wamefanya,waulizwe bila woga.Albert Kissimahttp://www.blogger.com/profile/17395730843653433393noreply@blogger.com4